Mnamo tarehe 7 mwezi wa pili mwaka wa elfu mbili na ishirini,wanafunzi wa chuo kikuu cha moi iliyoko katika kaunti la Uasin Gishu, eneo la Kesses, walijumuika kubaini viongozi watakao wawakilisha katika shule mbalimbali.
Asubuhi hiyo,umati wa wanafunzi ulionekana ukielekea katika vituo vya kupiga kura.

Waandalizi waligawa vituo vya kupigia kura ili kuepusha mirundiko ya wanafunzi wakati wa kupiga kura. Vituo hivyo vikiwa STUDENT’S CENTER na ICDC complex.

Wagombeaji walionyesha utulivu na nidhamu wakati wa kupiga kura na pia katika kipindi chote cha siasa. Lengo lao likiwa ni kudumisha amani na kuleta maendeleo katika nyadhfa wanayogombea. Hata hivyo,walizidi kuwahimiza wafuasi wao waje kwa wingi na kushiriki katika zoezi la kupiga kura.
Matokeo yalitangazwa adhuhuri hiyo na wafuatao ni miongoni wa walioshinda:
- Dennis Khaemba Sikuku
- Bolo Brian Ogembo(anafahamika kama Denzel Brian)
- Esther Ndunge
- Felix Kwemoi

Washindi hao watawakilisha wanafunzi katika baraza la wanafunzi ambapo watawachagua viongozi watakao ongoza,endeza na kudumisha baraza hilo la thelathini na tatu.

Matokea yalionekana kuwaridhisha wafuasi maana usiku huo,sherehe ziliandaliwa huku washindi wakibebwa juu kuonyesha ushindi wao.







And for the voters,they only require their school identification card,for them to vote.


